Ijumaa, 13 Julai 2018



KIVIPI FASIHI SIMULIZI NI MAMA WA FASIHI ANDISHI?

       Ngure(2003) anasema kuwa fasihi ni aina ya sanaa ambayo wasanii wake huonyesha ustadi wao katika kutumia maneno kisanii ili kuwasilisha ujumbe wao kwa wasomaji au jamii iliyonuiwa.
           Naye Mulokozi(1989) anasema, fasihi ni sanaa itumiayo lugha ili kufikisha ujumbe kwa jamii bila kujali kuwa imeandikwa au haijaandikwa.
          Kwa ujumla fasihi ni aina au kazi ya sanaa ambayo hutumia lugha katika uwasilishaji wake kwa hadhira lengwa ili kufikisha ujumbe uliokusudiwa bila kujali kuwa imeandikwa au haijaandikwa.
          Mulokozi(1996) anasema kuwa fasihi simulizi ni fasihi inayotungwa au kubuniwa kichwani na kuwasilishwa kwa hadhira kwa njia ya mdomo na matendo bila kutumia maandishi.Na anadai kuwa fasihi simulizi ni tukio linalofungamana muktadha au mazingira Fulani ya jamii.
         TUKI(2004)Fasihi simulizi ni kazi ya fasihi inayohifadhiwa na kurithishwa kutoka kizazi kimoja hadi kingine kwa nji aya mdomo kama vile hadithi,ngoma na vitendwili.
        Kwa ujumla fasihi simulizi ni ile kazi ya fasihi inayotungwa na kubuniwa katika kichwa cha binadamu na kuwasilishwa kwa hadhira au jamii lengwa kwa njia ya masimulizi ya mdomo na vitendo bila ya maandishi.
          Wamitila(2003) anasema fasihi andishi ni sanaa itumiayo maandishi kufikisha ujumbe kwa hadhira iliyo kusudiwa.
          Hivyo basi fasihi andishi ni aina au kazi ya sanaa ambayo hutumia maandishi kama njia kuu ya kufikisha ujumbe kwa jamii au hadhira lengwa iliyokusudiwa.
         Ni kweli na dhahiri kwamba fasihi simulizi ni mama wa fasihi andishi.Na hii ni kwa kuwa fasihi simulizi ndiyo ya mwanzo kuibuka kwani hii ilianza mara tu binadamu alivyoanza kupambana na mazingira yake.Fasihi  ya kipindi cha mwanzo ilijikita hasa katika masuala ya uzalisahaji mali ambapo nyimbo ziliimbwa ili kuchapuza kazi.Fasihi andishi iliibuka mara tu binadamu alivyogundua maandishi ndipo kazi mbalimbali za fasihi zilipoanza kuandikwa.Dai la kuwa fasihi simulizi ni mama wa fasihi andishi linathibitishwa na hoja zifuatazo:-
            Kwanza, dai hili linajidhihirisha katika tanzu za fasihi;tanzu za fashi simulizi zinafanana sana na zile za fasihi andishi.Hii ni kwa kuwa fasihi andishi imejichotea tanzu na vipera vyake katika fasihi simulizi.Mfano utanzu wa hadithi fupi.Hadithi fupi andishi zimetokana na hadithi fupi simulizi.Wanafasihi wengine wanauona utanzu huu kuwa ni wa fasihi simulizi kama vile Kingei na Catherin(2010:3) kama wanavyonukuliwa na samweil(2012:3).Samwel(2012:6),yeye anauchukulia utanzu huu wa hadithi fupi kuwa ni utanzu wa hadithi fasihi simulizi na pia andishi.Hivyo basi utanzu wa hadithi fupi andihshi umetoka na utanzu mmja wa fasihi andishi ambao ni utanzu wa masimulizi.
            Sio hayo tu,vilevile mitindo ya kazi fasihi simulizi;mtindo ni namna mwandishi anavyoumba kazi yake.Ngure(2003) anasema kuwa `tunaweza kutumia mfano wa Shaaban Robert katika kusadikika na kufikirika katika mitindo ya ngano zetu za `paukwa –pakawa ‘wakaishi raha mstarehe’.Ngule anasema kuwa hadithi hizi zinamtiririko mwepesi wa vituko uliofungamana na adili ya hadithi zenyewe.Mtindo huu niwa kifasihi simulizi.Hivyo basi,Shaaban Robert ametumia mtindo wa fasihi simulizi katika kuunda kazi yake ya fasihi andishi.Kwa maana hiyo fasihi andishi imechukua muundo wa fasihi simulizi.
               Vilevile suala la dhamira;dhamira ni kusudio la mtunzi wa kazi ya fasihi. Ngure(2003)anasema kuwa dhamira nyingi wanazozijadili waandishi wa leo zilikwishajadiliwa zamani katika fasihi simulizi.Na miongoni mwa dhamira hizo ambazo Ngure anazitaja ni pamoja na mapenzi,kisasi,harakati za kitabaka na unyonge wa mwanamke.Hii ni dhahiri kwamba dhamira za fasihi andishi zimetoka katika zile za fasihi simuizi.Ngure anaendelea kwa kusisitiza kuwa fasihi andishi haijafumbua dhamira mpya kabisa ila inaongezea maudhui mapya katika dhamira zizo hizo.
            Vilevile kipengele cha wahusika wa wao;hawa  ni wanyama,vitu,miti,watu na viumbe wengine ambao hubeba hulka na matendo ya binadamu.Wahusika ambao wanatumika katika fasihi simulizi ndio haohao wanaotumika katika fasihi andishi na kuwapa uhusika unaosawili matendo mbalimbali ya binadamu.Mfano hadithi za sungura kama Samweli(2012:20) anavyonukuu hurafa ya sungura na mkulima kutoka kwa Kanuri na wenzake(hakuna tarehe).Wahusika wake ni wanyama ambao hupewa uwezo wa kutenda kama binadamu ili kueleza hali halisi.Wahusika hawa wameingizwa katika kazi fasihi andishi.Wahusika kama watu hutumika katika fasihi simulizi na ndio hao hao wanaotumika sasa katika fasihi andishi.Hivyo ni dhahiri kwamba wahusika wa fasihi andishi wametokana na wahusika wa fasihi siumlizi.
              Hata hivyo muundo wa kazi hizo;muundo ni mtiririko na mpangilio wa visa na matukio katika kazi ya fasihi.Hurekelea msuko wa visa na matukio katika fasihi. Mara nyingi fasihi simulizi hutukia muundo wa moja kwa moja au muundo sahili.Mfano hadithi nyingi kama hekaya za Abunuwasi (Samwel 2012:21) zina muundo wa moja kwa moja.Yaani kisa huelezwa moja kwa moja bila kurejea nyuma au kurukia matukio.Fasihi andishi imechukua muundo huu wa moja kwa moja katika kuunda visa na matukio..Mfano Haji Gora Haji  ametumia muundo wa moja kwa moja katika riwaya yake ya Vuta n’Kuvute.

Jumatano, 26 Aprili 2017

TANZU ZA FASIHI ANDISHI






                                  TANZU ZA FASIHI ANDISHI 
                                       RIWAYA (NATHARI)
                                     USHAIRI (NUDHUMU)
                                           TAMTHILIYA (SANAA ZA MAONYESHO)
                                           FANI NA MAUDHUI KATIKA FASIHI 


Fani na maudhui katika fasihi ndio maumbo mawili makuu yanayobeba sanaa hii. 
                                                                         FANI
Fani ni ufundi unaotumiwa na msanii katika kufikisha ujumbe uliokusudiwa, fani sio ujumbe bali ni mfano wa kipaza sauti kinachotumika kufikisha ujumbe.
                                                            VIPENGELE VYA FANI
Fani inavipengele vingi, kila kipengele kina husika kipekee kwa kutofautiana na kipengele kingine. 

                                                       Vipengele vya fani ni pamoja na;
                                                                     a)   Muundo
 Kipengele hiki hutumiwa kueleza mpangilio wa kazi ya kifasihi. Kwa ufupi kwenye kipengele cha muundo tunaangalia umbo la kazi ya fasihi, mfano kazi yaweza kugawanywa katika sura mbalimbali, sura hizi ndizo ujenga muundo.
                                                                     b)  Mtindo
Williady (2015) mtindo ni mbinu za kipekee zinazomtofautisha msanii mmoja na mwingine. Mfano katika fasihi simulizi kipengele cha nyimbo hadhira inaweza kusikia wimbo kwa mara ya kwanza na kutambua wimbo huo umeimbwa na nani bila ya kuambiwa na mtangazaji, hii huweza kutokea pindi mwimbaji mashuhuri anayetumia mtindo wa peke yake katika sauti na mpangilio wa mashairi anapotoa wimbo mpya. Huu ndio huitwa mtindo. Katika fasihi andishi mtindo unaweza kujitokeza kwa njia za kipekee za mtunzi katika matumizi ya lugha, methali na misemo, msuko na mpangilio wa vina na mizani katika ushairi.
                                                                   c)   Mandhari
Williady (2015) Mandhari ni eneo au mazingira ya kweli au yakubuni ambayo hutumiwa na mwandishi katika kuwajenga wahusika na uhusika wao. 

                                                                    d)  Matumizi ya Lugha

Williady (2015) Matumizi ya lugha ni ustadi wa msanii katika kutumia lugha itakayoleta mvuto kwa wasomaji au wasikilizaji wa kazi ya fasihi.

Katika kutumia lugha msanii lazima azingatie kipengele cha uteuzi wa maneno yanayoendana na hadhira yake, maneno hayo ndiyo yatakayoleta mfungamanisho katika ya msanii, hadhira na ujumbe uliokusudiwa.

                                                                   e)   Matumizi ya tamathali za semi(usemi)

Williady (2015) Tamathali maanayake ni neon moja au kifungu cha maneno kilicho sukwasukwa na kufichwa maana.

Baadhi ya tamathali za semi katika Kiswahili ni pamoja na;
Tashibiha, sitiari, tafsida, tashihisi, chuku, kinaya,dhihaka, mbalagha,tabaini

                                                                    f)    Mbinu nyingine za kisanaa

Hapa huwa na mchanganyiko wa mbinu kadhaa katika usimulizi na silazima mbinu hizo zitumike zote kwa wakati mmoja. Mfano wa mbinu hizo ni pamoja na;

 Takriri, kuchanganya ndimi, tanakali sauti, taswira, lakabu, nahau na misemo
       
                                                                  e)   Wahusika

Williady (2015) wahusika ni viumbe hai au viumbe ambao si hai wanaobebeshwa majukumu na msanii ili kuwafikishia hadhira ujumbe uliokusudiwa.

                                                     MAUDHUI KATIKA FASIHI SIMULIZI

(williady: 2015) Maudhui ni jumla ya mawazo anayoyazungumzia msanii au mtunzi katika kazi ya fasihi.
Maudhui hujumuisha vipengele mbalimbali, kama vile;Dhamira, ujumbe, falsafa, mafunzo, migogoro na mtazamo.

TANBIHI: Kuna baadhi ya wataalamu wa lugha wanakiweka kipengele cha migogoro upande wa fani na kunabaadhi wanakiweka kipengele hiki upande wa maudhui. Mimi nakiweka upande wa maudhui kwa kuwa migogoro inabeba kwa kiasi kikubwa ujumbe kuliko ufundi.

                                                                      DHAMIRA

Dhamira ni shabaha kuu ya mtunzi wa kazi ya fasihi. Shabaha hii ukusudiwa ni nani wakumlenga nayo. Msanii anaweza kuwalenga kimaudhui watoto, wanawake, wasomi au watu wote katika jamii. Shabaha hii yaweza kuandikwa au kutongolewa kwa mdomo ikiwa na lengo la kupongeza, kuhimiza, kushauri, kutoa taarifa na kukosoa.

                                                                       UJUMBE

Ujumbe ni mawazo yanayotokana na dhamira, mawazo haya yaweza kujitokeza waziwazi au kwa kificho.

                                                                       FALSAFA

Falsafa ni hekima hekima ya mtunzi. Mtunzi huamini kuwa  kupitia imani hii jamii inaweza kupata suluhisho la matatizo yanayowakabili. Kwa mfano shekhe Shaaban Robert aliamini kuwa kila mwanajamii akiwa na utu basi haki na upendo vitapatikana kirahisi.

                                                                       MAFUNZO

Mafunzo ni nasaha anazotoa mtunzi ambazo huifundisha hadhira maadili Fulani. Maana ya mafunzo hutegemea namna hadhira inavyofasili nasaha hizo.

                                                                       MIGOGORO

Migogoro ni misuguano au mikinzano ama kutoelewana kati ya pande mbili au zaidi ndani ya kazi za fasihi.

                                                              AINA ZA MIGOGORO

                                                               Mgogoro kati ya mtu na mtu
                                                              Mgogoro kati ya mtu na jamii
                                                              Mgogoro kati ya jamii na jamii 
                                                              Mgogoro wa nafsi
 
                                                                      VI. MTAZAMO
Mtazamo na jinsi mwandisi anavyotazama na kuyachukulia matukio katika ulimwengu na athari zake kwa wanajamii. Mfano waandishi wengi wa mashairi wanamtazamoa huu “Kuibuka kwa maovu mengi duniani kwasasa  ni matokeo ya binadamu kuasi dini.
mawasiliano:
0657882566
0742508002

KIVIPI FASIHI SIMULIZI NI MAMA WA FASIHI ANDISHI?        Ngure(2003) anasema kuwa fasihi ni aina ya sanaa ambayo wasanii wake huonyes...