Jumatano, 26 Aprili 2017

TANZU ZA FASIHI ANDISHI






                                  TANZU ZA FASIHI ANDISHI 
                                       RIWAYA (NATHARI)
                                     USHAIRI (NUDHUMU)
                                           TAMTHILIYA (SANAA ZA MAONYESHO)
                                           FANI NA MAUDHUI KATIKA FASIHI 


Fani na maudhui katika fasihi ndio maumbo mawili makuu yanayobeba sanaa hii. 
                                                                         FANI
Fani ni ufundi unaotumiwa na msanii katika kufikisha ujumbe uliokusudiwa, fani sio ujumbe bali ni mfano wa kipaza sauti kinachotumika kufikisha ujumbe.
                                                            VIPENGELE VYA FANI
Fani inavipengele vingi, kila kipengele kina husika kipekee kwa kutofautiana na kipengele kingine. 

                                                       Vipengele vya fani ni pamoja na;
                                                                     a)   Muundo
 Kipengele hiki hutumiwa kueleza mpangilio wa kazi ya kifasihi. Kwa ufupi kwenye kipengele cha muundo tunaangalia umbo la kazi ya fasihi, mfano kazi yaweza kugawanywa katika sura mbalimbali, sura hizi ndizo ujenga muundo.
                                                                     b)  Mtindo
Williady (2015) mtindo ni mbinu za kipekee zinazomtofautisha msanii mmoja na mwingine. Mfano katika fasihi simulizi kipengele cha nyimbo hadhira inaweza kusikia wimbo kwa mara ya kwanza na kutambua wimbo huo umeimbwa na nani bila ya kuambiwa na mtangazaji, hii huweza kutokea pindi mwimbaji mashuhuri anayetumia mtindo wa peke yake katika sauti na mpangilio wa mashairi anapotoa wimbo mpya. Huu ndio huitwa mtindo. Katika fasihi andishi mtindo unaweza kujitokeza kwa njia za kipekee za mtunzi katika matumizi ya lugha, methali na misemo, msuko na mpangilio wa vina na mizani katika ushairi.
                                                                   c)   Mandhari
Williady (2015) Mandhari ni eneo au mazingira ya kweli au yakubuni ambayo hutumiwa na mwandishi katika kuwajenga wahusika na uhusika wao. 

                                                                    d)  Matumizi ya Lugha

Williady (2015) Matumizi ya lugha ni ustadi wa msanii katika kutumia lugha itakayoleta mvuto kwa wasomaji au wasikilizaji wa kazi ya fasihi.

Katika kutumia lugha msanii lazima azingatie kipengele cha uteuzi wa maneno yanayoendana na hadhira yake, maneno hayo ndiyo yatakayoleta mfungamanisho katika ya msanii, hadhira na ujumbe uliokusudiwa.

                                                                   e)   Matumizi ya tamathali za semi(usemi)

Williady (2015) Tamathali maanayake ni neon moja au kifungu cha maneno kilicho sukwasukwa na kufichwa maana.

Baadhi ya tamathali za semi katika Kiswahili ni pamoja na;
Tashibiha, sitiari, tafsida, tashihisi, chuku, kinaya,dhihaka, mbalagha,tabaini

                                                                    f)    Mbinu nyingine za kisanaa

Hapa huwa na mchanganyiko wa mbinu kadhaa katika usimulizi na silazima mbinu hizo zitumike zote kwa wakati mmoja. Mfano wa mbinu hizo ni pamoja na;

 Takriri, kuchanganya ndimi, tanakali sauti, taswira, lakabu, nahau na misemo
       
                                                                  e)   Wahusika

Williady (2015) wahusika ni viumbe hai au viumbe ambao si hai wanaobebeshwa majukumu na msanii ili kuwafikishia hadhira ujumbe uliokusudiwa.

                                                     MAUDHUI KATIKA FASIHI SIMULIZI

(williady: 2015) Maudhui ni jumla ya mawazo anayoyazungumzia msanii au mtunzi katika kazi ya fasihi.
Maudhui hujumuisha vipengele mbalimbali, kama vile;Dhamira, ujumbe, falsafa, mafunzo, migogoro na mtazamo.

TANBIHI: Kuna baadhi ya wataalamu wa lugha wanakiweka kipengele cha migogoro upande wa fani na kunabaadhi wanakiweka kipengele hiki upande wa maudhui. Mimi nakiweka upande wa maudhui kwa kuwa migogoro inabeba kwa kiasi kikubwa ujumbe kuliko ufundi.

                                                                      DHAMIRA

Dhamira ni shabaha kuu ya mtunzi wa kazi ya fasihi. Shabaha hii ukusudiwa ni nani wakumlenga nayo. Msanii anaweza kuwalenga kimaudhui watoto, wanawake, wasomi au watu wote katika jamii. Shabaha hii yaweza kuandikwa au kutongolewa kwa mdomo ikiwa na lengo la kupongeza, kuhimiza, kushauri, kutoa taarifa na kukosoa.

                                                                       UJUMBE

Ujumbe ni mawazo yanayotokana na dhamira, mawazo haya yaweza kujitokeza waziwazi au kwa kificho.

                                                                       FALSAFA

Falsafa ni hekima hekima ya mtunzi. Mtunzi huamini kuwa  kupitia imani hii jamii inaweza kupata suluhisho la matatizo yanayowakabili. Kwa mfano shekhe Shaaban Robert aliamini kuwa kila mwanajamii akiwa na utu basi haki na upendo vitapatikana kirahisi.

                                                                       MAFUNZO

Mafunzo ni nasaha anazotoa mtunzi ambazo huifundisha hadhira maadili Fulani. Maana ya mafunzo hutegemea namna hadhira inavyofasili nasaha hizo.

                                                                       MIGOGORO

Migogoro ni misuguano au mikinzano ama kutoelewana kati ya pande mbili au zaidi ndani ya kazi za fasihi.

                                                              AINA ZA MIGOGORO

                                                               Mgogoro kati ya mtu na mtu
                                                              Mgogoro kati ya mtu na jamii
                                                              Mgogoro kati ya jamii na jamii 
                                                              Mgogoro wa nafsi
 
                                                                      VI. MTAZAMO
Mtazamo na jinsi mwandisi anavyotazama na kuyachukulia matukio katika ulimwengu na athari zake kwa wanajamii. Mfano waandishi wengi wa mashairi wanamtazamoa huu “Kuibuka kwa maovu mengi duniani kwasasa  ni matokeo ya binadamu kuasi dini.
mawasiliano:
0657882566
0742508002

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KIVIPI FASIHI SIMULIZI NI MAMA WA FASIHI ANDISHI?        Ngure(2003) anasema kuwa fasihi ni aina ya sanaa ambayo wasanii wake huonyes...