MAANA YA FASIHI NA UCHAMBUZI WA VIPERA VYAKE
Williady, (2015) Fasihi ni tawi moja wapo la sanaa linalotumia lugha katika kuwasilisha ujumbe wa mdomo au wa maandishi.
Wamitila
(2004) Fasihi ni sanaa inayotumia luha na ambayo hujishughulisha na binadamu
pamoja na maisha yake na huathri, hugusa au huacha athari fulanina hupatikana
katika umbo ambalo linatambuliwa na jamii Fulani.
Kwakuwa
fasihi ni aina ya sanaa, ni vyema mwanafunzi akajua pia maana ya sanaa.
MAANA YA SANAA
(Williady:
2015) Sanaa ni ujuzi au ufundi wenye kuleta manufaa kwa uma.
UMBO LA SANAA
Tunaposema
umbo la sanaa tunamaanisha matawi yanayojenga sanaa. Matawi hayo nipamoja na;
Fasihi,
maonyesho, ususi, uhunzi, ufumaji, utarizi, uchongaji, ufinyanzi, uchoraji na
muziki.
AINA/ KUMBO/ TANZU ZA FASIHI
Katika
kumbo ya fasihi na taaluma zake kuna aina kuu mbili za fasihi, ambazo ni;
Fasihi Simulizi
Fasihi Andishi
TOFAUTI KATI YA FASIHI SIMULIZI NA FASIHI ANDISHI
Namna ya uwasilishaji wake. Fasihi simulizi huwasilishwa kwa njia yam
domo wakati fasihi andishi uwasilishwa kwa njia ya maandishi.
Mabadiliko. Fasihi simulizi huweza kupokea mabadiliko ya papo kwa papo
wakati fasihi andishi hurekebishwa baada ya toleo jipya.
Utendaji wake kwa hadhira na fanani. Hadhira na fanani katika fasihi
simulizi huwa ni yakiutendaji, wasikilizaji wanaweza kuchangia mawazo
kwa kutoa maoni, kuuliza maswali au kushadadia masimulizi ya
fanani. Fasihi andishi hadhira hawawezi kuchangia lolote.
Ukongwe. Fasihi simulizi niyazamani zaidi, ilianza wakati mwanadamu
alipoanza kutumia mdomo katika mawasiliano. Fasihi andishi ilianza pindi
maandishi yalipobuniwa.
Vidato na elimu. Fasihi simulizi haiitaji mtu ajue kusoma ama kuandika,
inamuhitaji mtu mwenye uwezo wa kuzungumza. Fasihi andishi
inamhitaji mtu anayejua kuandika na kusoma.
Umiliki. Fasihi simulizi inamilikiwa na jamii nzima wakati fasihi
andishi humilikiwa na mwandishi aliyeandika na kupiga chapa kazi hiyo.
Idadi ya tanzu. Fasihi simulizi inatanzu nyingi zaidi kuliko fasihi
andishi.
Kuhifadhi. Hapo kale fasihi simulizi ilihifadhiwa kichwani, kwa sasa
fasihi simulizi yaweza kuhifadhiwa katika vinasa sauti, kaseti na santuri.
Fasihi andishi yenyewe huifadhi wake ni kwa njia ya maandishi.
Mwingiliano wa tanzu kwa kiasi. Fasihi simulizi huweza kuingiliwa kwa
kiasi kikubwa na tanzu nzingine kama vile methali, vitendawili, nyimbo na
nahau wakati fasihi andishi huweza kuingiliwa na tanzu nyingine kwa kiasi
kidogo.
UFAFANUZI WA AINA ZA FASIHI
1.Fasihi simulizi
Fasihi
simulizi ni aina ya fasihi inayotumia mdomo na utendaji wa viungo vya mwili
katika kuwasilisha maudhui ya fanani kwa hadhira iliyokusudiwa.
TANZU
ZA FASIHI SIMULIZI
Hadithi, uigizaji, ushairi na semi
VIPERA VYA HADIDHI
Ngano, vigano, hekaya, soga,
tarihi, visa, visasili, shajara, istiala, michapo na mbazi
VIPERA VYA UIGIZAJI
Miviga, michezo ya jukwaani,
majigambo, utani, vichekesho, ngonjera, mgomezi na
mazungumzo
mazungumzo
VIPERA VYA USHAIRI
Nyimbo, maghani,
ngonjera, mashairi, tenzi na tendi
AINA ZA NYIMBO
Bembezi, nyimbo za mapenzi,
nyiso, nyimbo za jadi, nyimbo za harusi, nyimbo za watoto
nyimbo za sifa, nyimbo za kampeni, nyimbo za maombolezo na nyimbo za chombezi.
nyimbo za sifa, nyimbo za kampeni, nyimbo za maombolezo na nyimbo za chombezi.
VIPERA VYA SEMI
Methali, misimu,
lakabu, nahau, vitendawili. utani, misimu, mafumbo, masaguo, mizungu na
misemo
misemo
MAJUKUMU / DHIMA ZA FASIHI SIMULIZI KATIKA JAMII
Kuelimisha,
kuburudisha, kusisimua, ukombozi, kutoa mwongozo kwa jamii, kutunza amali
za jamii (historia na utamaduni), kujuza na kuunganisha vizazi nz vizazi, kufundisha,
kudumisha uhusiano, kudumisha ushirikiano na kukuza stadi za lugha
za jamii (historia na utamaduni), kujuza na kuunganisha vizazi nz vizazi, kufundisha,
kudumisha uhusiano, kudumisha ushirikiano na kukuza stadi za lugha
MAMBO MUHIMU YA KUZINGATIA KATIKA USIMULIZI WA HADITHI
Ili
msimuliaji aweze kutongoa au kusimulia hadithi kwa usahihi inampasa awe na
weledi wa kutosha juu ya mbinu za kusimulia hadithi. Mbinu hozo ni hizi;
A) Dhima na maudhui
Msimuliaji
wa hadithi anapaswa kujua lengo kuu (dhima) la hadithi yake. Vilevile
msimuliaji anapaswa kujua maudhui ambayo ni jumla ya mambo yote yanayopelekea
hadithi kutiririka vizuri kwenye mkondo wake.
B) Msuko
Msuko
wa matukio kwa jina jingine unafahamika kama muundo. Kipengele hiki cha muundo
kinahusu mpangilio wa hadithi kuanzia mwanzo mpaka mwisho.
C) Kusisimua
Kusisimua
ni mbinu inayovuta umakini kwa watu. Msimuliaji anaweza kutumia mbinu kadhaa
zitakazo msisimusha msomaji, mbinu kama vile taharuki, miguno na kelele za
kutisha.
D) Urudufishaji
Huu
ni urudiaji rudiaji katika fasihi simulizi. Mara nyingi msimuliaji anashauriwa
kurudia rudia maneno, falsafa, nahau au vitendawili vilivyobeba lengo kuu la
hadithi yake.
E) Chombezo
Chombezo
ni kipengele kidogo kinacho elezwa na mtambaji wa hadithi chenye lengo la
kupunguza ukakasi ama ukalia ama vitisho vilivyotokana na maudhui ya hadithi
Fulani.
F) Nyimbo
Nyimbo
zina kazi nyingi katika masimulizi ya hadithi. Moja wapo ya matumizi hayo ni
kama vile kuondoa uchovu kwa wasikilizaji, kuvuta usikivu, kuwakaririsha
hadhira falsafa au lengo kuu la hadithi hiyo.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni